Aina hii ya safari zetu bila kujali ndiyo mara nyingi inatuletea hatari ya maisha hasa inapotokea ajali japo kwa bahati mbaya.Katika picha inaonyesha abiria na mizigo yao wakiwa wanasubiri chombo kikae sawa waendelee na safari yao kati ya Sumbawanga mjini kuelekea Bonde la Ziwa Rukwa, hali hiyo ni hatari kwa watu na mizigo lakini inajitokeza kutokana na ugumu wa usafiri katika maeneo mengi ya vijijini.
'Traffic tuwe wakali inapobidi ili kukemea hali hii, maana bora kinga kuliko tiba'
Picha na Mussa Mwangoka,Sumbawanga.